Wamesema licha ya Bunge kuongozwa na kanuni, wakati mwingine viongozi hao wa Bunge wanatumia kanuni hizo kuwapendelea wabunge wa CCM, huku wakieleza kuwa licha ya wabunge wa chama hicho kutukana, hawakupewa adhabu yoyote.
Jumatano ya wiki hii, Ndugai aliwasimamisha Tundu Lissu (Singida
Mashariki), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Mchungaji Peter Msigwa
(Iringa Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiah Wenje (Nyamagana) na
Godbless Lema wa Arusha Mjini kutohudhuria Bunge kwa siku tano kutokana
na alichokiita kufanya vurugu ndani ya Bunge.
Uamuzi huo wa Spika Makinda ulikuja baada ya
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kumtaka
Ndugai aeleze alitumia kanuni gani kuwasimamisha wabunge hao.
Kwa habari zaidi www.mwananchi.co.tz
Kwa habari zaidi www.mwananchi.co.tz
No comments:
Post a Comment