BURUDANI

Sekeleti Wa Zambia Kushiriki Pasaka


MWIMBAJI wa muziki wa Injili kutoka Zambia, Ephraim Sekeleti Mutalange amethibitisha kushiriki tamasha la Pasaka litakalofanyika Sikukuu ya Pasaka Aprili 8 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ambaye ni Mkurugenzi wa Msama Promotions, waandaaji wa tamasha hilo, Sekeleti amekubali kushiriki.Msama alisema Dar es Salaam jana kuwa mwimbaji huyo wa nyimbo za kumsifu Mungu atatua nchini akiwa na albamu zake za Acha Kulia na Mungu Mwenyewe.Msama alizitaja baadhi ya nyimbo zilizomo kwenye albamu hiyo kuwa ni Uniongoze na Kidonge cha Yesu. Baada ya kutikisa Uwanja wa Taifa, mashambulizi mengine yatahamia kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma Aprili 9 mwaka huu."Sekeleti ameomba mashabiki wajitokeze kwa wingi, hivyo ni nafasi nzuri kwa Watanzania kufika kumshuhudia mwimbaji huyo," alisema Msama.Aliongeza kwamba Sekeleti atakuja nchini na waimbaji wake 10 na ataimba 'live' siku hiyo ambayo mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.Sekeleti ni mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili nchini Zambia, alizaliwa mwaka 1983 katika mji wa Kalulushi, Zambia. Alimaliza elimu yake ya sekondari katika Shule ya Kalulushi mwaka 2001.Sekeleti ni mtoto wa pili kutoka mwisho kati ya watoto sita. Aliingia kwenye muziki wa injili tangu akiwa kinda huku alifundishwa kupiga kinanda na mmisionari.Tamasha la Pasaka la mwaka huu lina malengo ya kuchangisha fedha kwa ajili ya watoto yatima na kuwasaidia mitaji ya biashara wajane wasiojiweza.Kiingilio katika tamasha hilo kimetengwa katika kategoria tatu na kitakuwa sh. 2,000 kwa watoto, sh. 5,000 kwa viti vya kawaida na viti maalumu sh. 10,000.Mbali na Sekeleti, wasanii wengine wa nyimbo za Injili watakaopamba tamasha hilo ni Rebecca Malope, Rose Muhando, Christina Shusho, Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, Solomon Mukubwa, Anastazia Mukabwa, Atosha Kissava na kundi la Glorious Celebration.Pia kwaya mahiri ya Kinondoni Revival inayotamba na albamu yao mpya ya Mtu wa Nne, inatarajia kutumbuiza katika tamasha la Pasaka na Mwinjilisti Faraja Ntaboba kutoka DRC.Tamasha la Pasaka la mwaka huu litashirikisha waimbaji wa nyimbo za Injili kutoka nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Afrika Kusini na Zambia.

Solomn Mukubwa Kutumbuiza Tamasha La Pasaka


Na Mwandishi Wetu

KATIKA matamasha ya Pasaka mwaka 2010 na 2011, yaliyopambwa kwa muziki wa Injili kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam, kusherehekea Sikukuu ya Pasaka, nyoyo za mashabiki zilikongwa na waimbaji kochokocho waliotumbuiza.

Lakini kivutio kikubwa walikuwa ni mwimbaji wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) anayeishi Kenya, Solomon Siaka Mukubwa na Rose Muhando, ambao mara kwa mara kelele za mashabiki zilisikika wakitaka kila mmoja aendelee kuwapa burudani.

Mbali ya Rose Muhando ambaye wimbo wake wa Nibebe uliteuliwa kuwa Wimbo Bora wa Mwaka 2009 kupitia televisheni ya Taifa, TBC1 na Mukubwa, wasanii wengine walioshiriki na kufanya vizuri ni Flora Mbasha na Upendo Nkone.

Waimbaji wengine ni Bahati Bukuku, Jennifer Mgendi, Geraldine Oduor, Enock Jonas, na kundi la muziki wa Injili la Upendo la Kijitonyama, Dar es Salaam.

Lakini Mukubwa na Rose ndio waliokuwa kivutio zaidi kutokana na kushangiliwa kwa nguvu. Mukubwa anasema hamasa aliyoipata mwaka juzi na mwaka jana ndiyo inampa msukumo zaidi wa kuendelea kukonga nyoyo za mashabiki katika tamasha la mwaka huu.

Tamasha la mwaka huu litafanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Aprili 8, kisha litarindima kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Aprili 9, ambayo itakuwa Jumatatu ya Pasaka.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama anasema kwa vile tamasha la mwaka jana lilikuwa la mafanikio makubwa, anaamini mwaka huu watavuka malengo ya kukusanya fedha kwa ajili ya watoto yatima na kuwasaidia mitaji ya biashara wajane wasiojiweza.

Wasifu wa Mukubwa

Mukubwa ni mlemavu wa mkono mmoja wa kushoto anaodai umekuwa katika hali hiyo kutokana na kudhuriwa kwa uchawi na mama yake wa kambo alipokuwa na umri mdogo.

Anasema akiwa na miaka 12, alipata matatizo hayo kwa kutokea uvimbe wa ajabu na hakuna aliyejua tatizo lilikuwa nini, lakini walibaini kuwa ni mama yake wa kambo ndiye alimroga kutokana na wivu.

Mukubwa aliyetamba na wimbo wa 'Mfalme wa Amani', anabainisha kwamba aliugua kwa miaka mitatu na alihaha huku na huko hospitalini hadi kwa waganga wa kienyeji kusaka tiba, lakini hakufanikiwa.

Kwa mantiki hiyo, alifikia uamuzi wa kukatwa mkono kwa vile ulikuwa umeharibika.

Mukubwa anasema mama yake huyo wa kambo alikiri kumroga baada ya kuokoka, hivyo alimsamehe. Hata hivyo, anasema mkono huo aliokatwa haumzuii kumuimbia Mungu.

Mukubwa anasema alihamia Kenya kutokana na msaada wa mwimbaji wa nyimbo za Injili, marehemu Angela Chibalonza, aliyekuwa mshauri wake.

Mukubwa amezaliwa kwenye familia ya watoto tisa, wanaume saba na wanawake wawili, yeye akiwa wa kwanza, ameoa kwa alifunga ndoa na Betty Japhet, Machi mwaka 2010.

Mwimbaji huyo wa nyimbo za kumsifu Mungu mwenye ulemavu wa mkono mmoja, hivi sasa anatamba na albamu yake mpya ya Usikate Tamaa, ambayo anaamini itamng'arisha katika tamasha hilo.

Nyimbo zilizomo kwenye albamu hiyo ya Usikate Tamaa ni Usikate Tamaa, Mungu Wangu Nitetee, Niko na Yesu, Mke Si Nguo, Moyo Tukuza Bwana, Chunga Ahadi Yako na Yesu Jina Zuri.

Mukubwa anayeishi Kenya, amewahi kutoa albamu mbili ambazo ni Sijaona Rafiki na Mungu Mwenye Nguvu.

Sijaona Rafiki Kama Yesu ambayo ni albamu yake ya kwanza ina nyimbo za Uwe Nami Bwana, Sijaona Rafiki Kama Yesu, Nitayainua Macho, Matendo ya Mungu, Bwana Wastahili na Yesu Kimbilio.

Albamu yake ya pili ya Mungu Mwenye Nguvu ina nyimbo za Mungu Mwenye Nguvu, Mkono wa Bwana, Mfalme wa Amani, Siku Moja, Tabia Ina Dawa na Roho Yangu Ikuimbie.

Wengine watakaoshiriki

Mbali na Mukubwa, wengine waliothibitisha kushiriki tamasha hilo litakalofanyika Sikukuu ya Pasaka ni Rose Muhando, Anastazia Mukabwa, Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, Christina Shusho, Atosha Kissava, Mwinjilisti Faraja Ntaboba kutoka DRC na kundi la Glorious Celebration.

Pia kwaya mahiri ya Kinondoni Revival inayotamba na albamu yao mpya ya Mtu wa Nne, inatarajia kutumbuiza katika tamasha la Pasaka. Mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

Nyimbo zilizomo kwenye albamu ya Kinondoni Revival ni Mtu wa Nne, Imekwisha, Chukua Hatua, Mtafuteni Bwana, New Season, Hakikisha, Ninakushukuru na Dini Iliyo Safi.

Pia kwaya hiyo ya Kinondoni Revival imewahi kutamba na albamu yao ya Kilio cha Mcha Mungu yenye nyimbo nane za Kilio cha Mcha Mungu, Kwanini Unataka Kujiua, Ayubu II, Vumilia Kidogo, Nafsi Yangu, Natamani Kwenda Mbinguni, Ndugu Yetu Twakutafuta na Twalilia Tanzania ambazo pia wameahidi wataziimba.

Msama anasema baada ya waimbaji hao kutikisa Uwanja wa Taifa, mashambulizi mengine yatahamia kwenye Uwanja wa Jamhuri, Dodoma Aprili 9 mwaka huu.

Kiingilio katika tamasha hilo kimetengwa katika kategoria tatu na kitakuwa sh. 2,000 kwa watoto, sh. 5,000 kwa viti vya kawaida na viti maalumu sh. 10,000.

Tamasha la Pasaka la mwaka huu pia litashirikisha waimbaji wa nyimbo za Injili kutoka nchi za Uganda, Rwanda, Afrika Kusini na Zambia. Pia kutakuwa na kwaya na vikundi vya burudani.

Jana na Leo


Kipanya Bwana!




MSONDO NGOMA KUENDELEA KUMTAMBULISHA SHABANI LENDI WIKI HII


BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo ngoma inatarajia kutoa burudani katika jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya kumtambulisha mwana mziki wao mpya Shabani Lendi.

Akizungumza Dar es Salaam Leo, Msemaji wa bendi hiyo Rajabu Mhamila 'Super D' alisema, baada ya kuwa Zanzibar na kutoa burudan kwa kumtambulisha Msanii huyo.


Sasa imepanga kumtambulisha siku ya Alhamisi ambapo watakuwa Kilimani Pub, Stakishari,Ijumaa Lidaz Clab, Kinondoni, Jumamosi TCC Klabu na Jumapili watakuwa katika ukumbi wa Max Bar Ilala Bungoni kwa ajili ya kumtambulisha Kikamilifu msanii huyo.


Super D amewataka wakazi wa Dar es Salaam na Mikoa ya Jirani kuhudhuria kushuhudia burudan hiyo watakayoitoa ikiwa ni pamoja kusikia nyimbo zao mpya ambazo ni miongoni mwa nyimbo zitakazo kuwa katika albamu yao mpya ya mwaka huu ikiwa ni pamoja kusikiliza nyimbo zao za zamani.

Alizitaja nyimbo hizo mpya kuwa ni Suluu ya Shabani Dede,Nadhiri ya Mapenzi ya Juma Katundu, Mjomba, Dawa ya deni kulipa na lipi jema ambapo albamu hiyo inatarajia hivi karibuni.



Mzee Hatari anayevunja mbavu
Mzee Ojwang aliye kaa kwenye kiti

Na Mwandishi wetu
Kicheko ndio dawa ya asilia ambapo kulingana na wataalamu, inaweza ikaongeza maisha ya mhusika kwa miaka kadha.

Nchini Kenya na Afrika Mashariki kwa ujumla, mwigizaji msifika Mzee Ojwang Hatari anafahamu vyema haya na ndiposa kwa zaidi ya miaka 40, amekuwa mstari wa mbele kuwasisimua mashabiki wake kwa uigizaji na filamu tofauti ambazo ajihusisha nazo

Kwa watazamaji wa televisheni, Ojwang ambaye huigiza katika lafudhi ya kabila la Kijaluo hahitaji kutambulishwa. Majina yake kamili ni Benson Wanjau Karira ambaye ni

Mkikuyu lakini kutokana na mapenzi ya uigizaji kama Mjaluo, alijitwiga jina Ojwang Hatari. Sio majina tu yanayomfananisha na mjaluo bali pia namna anavyovalia- aina ya kofia inayohusishwa mno na viongozi wengi wa jamii ya Kiluo akiwemo Waziri Mkuu Raila Odinga .

Ojwang hahitaji kutambulishwa kwa mashabiki wake kwani amekuwa kwenye televisheni, hafla za umma na pia kumbi tofauti za burudani kwa lengo la kuwatumbuiza mashabiki. Kwa mzee Ojwang, umri si hoja kwani anahisi safari yake kwenye sanaa ndiposa inang'oa nanga.

Umri huenda umenisonga lakini ukweli wa mambo ni kwamba sasa ninajihisi mwenye nguvu zaidi. Ninataka kuwatumbuiza mashabiki wangu kuliko jinsi nimekuwa nikifanya awali,

alisema mzee Ojwang ambaye huigiza katika kipindi cha Vitimbi kwenye kituo cha KBC. Waigizaji wengine wanaojitahidi kufuata nyayo zake za uigizaji ni pamoja na Papa Shirandula wa televisheni ya Citizen na Mogaka ambaye huigiza kwenye KBC.Mchezo wa Vitimbi umekuwa kikiperushwa kila wiki kwa zaidi ya miaka 30 iliyopita huku Ojwang akicheza nafasi ya mhusika mkuu sawa sawa na 'mkewe',

Mama Kayai na Mogaka.Iwapo ulidhani kwamba Mzee Ojwang anajiandaa kustaafu kwenye ulingo wa utumbuizaji, basi tafakari tena kwani anasema kwamba ameimarika zaidi ikilinganishwa na awali.

Uigizaji hauna kustaafu. Mtu anaweza kujiondoa kutokana na kushindwa kuendelea kufanya kazi hiyo lakini sio sababu ya umri, alieleza mzee ambaye umachachari wake kwenye steji huwachekesha wengi.

Mimi si Ojwang, iwapo unahitaji kuzungumza na Ojwang basi, itabidi uelekee KBC. Hapa mimi ni Benson Wanjau, " alisema mwigizaji huku tukipiga kambi katika mkahawa jijini Nairobi kwa mahojiano

Usimwone hivi ukadhani ni mzee asiyeweza kutangamana na vijana wa siku hizi. Ojwang anafahamu mno sheng ambayo huitumia kuwavutia vijana.

Nimezaliwa, kulelewa na kuishi Eastlands miaka yote na hivyo hakuna nisilolifahamu kuhusiana na sheng, alieleza mwigizaji aliyezaliwa katika mtaa wa Pumwani na kusoma Pumwami Missionary Church.

Akiwa mdogo, alijihusisha zaidi na masuala ya soka na hakufahamu kwamba wakati fulani angekuwa mwigizaji wa kutajika zaidi.

Ilikuwa vipi akapata jina Ojwang ambalo amekuwa akilitumia katika uigizaji.

Kabla ya kuanza kuigiza kwenye televisheni, nilikuwa mfanyakazi wa White Rose Drycleaners. Nilikuwa mcheshi mno bali na kuvalia kofia inayohusishwa na Wajaluo na ndiposa mwenzangu akanibandika jina Ojwang,

alikumbuka mwigizaji ambaye miaka miwili iliyopita, alikuwa Amerika kwenye shoo iliyofahamika kama Legend Tour iliyowashirikisha waigizaji wa Redykulass.

Iwapo orodha ya waigizaji wa kwanza humu nchini itaandaliwa, basi Ojwang aliye na watoto wawili na wajukuu wawili, atakuwa wa kwanza. Mbali na Vitimbi, amewahi kushiriki katika vipindi vya Darubini, Je, Huu ni Ungwana na Vioja Mahakamani.
Kipindi cha Vitimbi kilichukua nafasi ya Darubini kilichokuwa kikiperushwa hewani hadi 1985.

Baadhi ya waigizaji ambao wamewahi kuigiza na Ojwang kwenye Vitimbi ni pamoja na Amka Twende (Benjamin Otieno), Othorong'ong'o (Joseph Anyona), Mutiso (Kimunyo Mbuthia), Masanduku arap Simiti (Sammy Muya), Wariahe (Said Mohammed Said) na Otoyo Obambla (Samuel Mwangi).

Kutokana na uigizaji wake, Ojwang amejumuika na watu maarufu serikalini ikiwa ni pamoja na rais mstaafu Daniel Moi.

Katika kila hafla za kitaifa, kikundi cha Vitimbi hakikosi kutumbuiza.Kutokana na kuishi na kuwa kwenye burudani kwa muda mrefu, Ojwang ameona mengi na ndiposa anawashauri waigizaji wanaoanza kibarua hiki kuwa watulivu.

Kinyume na awali, sasa hivi taaluma hii inaheshimiwa na iwapo wahusika watakuwa wavumilivu, Bila shaka watapiga hatua kubwa mno, " anasema Ojwang'.

Gospel Live Ndani Pasaka


Na Mwandishi Wetu
KUNDI la muziki wa Injili la Glorious Celebration Spirit of Praise 'Gospel Live' nalo limejitosa kushiriki tamasha la Pasaka linalofanyika kila mwaka kwa kuandaliwa na Kampuni ya Msama Promotions ya Dar es Salaam.

Kundi hilo linalotamba na albamu ya Niguse, limethibitisha kushiriki tamasha hilo, hivyo kuzidi kufanya wigo wa tamasha hilo kupanuka zaidi kwa kushirikisha wasanii nguli.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema kundi la Glorious Celebration Spirit of Praise limeahidi kukonga nyoyo za mashabiki watakaohudhuria.

Tamasha hilo linatarajiwa kurindima Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Aprili 8 mwaka huu na pia litafanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Aprili 9 mwaka huu.

Glorious hivi sasa wanatamba na albamu ya Niguse yenye nyimbo za Unaweza Yesu, Ee Roho, Juu ya Mataifa, Mawazo, Ameni Haleluya, Nafsi Yangu, Nakupenda Yesu, Usilie na Niguse uliobeba jina la albamu.

Msama alisema mbali na Glorious, waimbaji wengine waliothibitisha kushiriki mpaka sasa ni Upendo Kilahiro, Upendo Nkone na Atosha Kissava kutoka Mkoa wa Iringa.

"Tunaboresha mambo mengi kuliko miaka iliyopita, waimbaji mwaka huu watakuwa wachache kiasi wakiwamo wa kutoka mataifa mengine ya Afrika... hiyo yote tumefanya ili kukidhi matakwa ya wapenzi wa muziki wa injili.

"Mbali na Tanzania, pia tutakuwa na waimbiaji kutoka Kenya, Uganda, Zambia, Afrika Kusini, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo katika tamasha hilo la nyimbo za injili za kumsifu Mungu.

"Waimbaji wengi maarufu wa muziki wa injili watakuwepo, tumejipanga vizuri kuhakiksha tamasha hili linakuwa gumzo kila mahali.

"Wapendwa wajiandae kushiriki kwa wingi kwani watashiba kiroho kwa vile kutakuwa na waimbaji wengi wenye hamasa ya kiroho," alisema Msama.

Msama alisema lengo la kuwajumuisha wasanii hao ni kutaka kulifanya tamasha hilo kuwa tofauti na miaka mingine.

Alisema tamasha hilo litakuwa na kiingilio cha chini zaidi (kitatangazwa wiki ijayo), ili kila mmoja ahudhurie na kupata baraka kutoka kwa waimbaji hao wanaomsifu Mungu


Msondo Yaibomoa Sikinde
Kiongozi wa bendi ya Msondo, Saidi Mabela (kulia) akimkabidhi Saxaphone msanii mpya wa bendi hiyo Shabani Lendi Dar es Salaam leo, baada ya kuingia mkataba wa miaka miwili akitokea bendi ya Sikinde katikati ni Meneja wa bendi hiyo Saidi Kibiliti.

No comments:

Post a Comment