Sunday, February 19, 2012

DKT. BILLAL AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA AFYA INYONGA LEO, AWAASA KINAMAMA WAJAWAZITO KUJIFUNGULIA KWENYE KITUO HICHO


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Billal akiweka jiwe la msingi katika Kituo Kikuu cha Afya Tarafa ya Inyonga Leo. Kituo hicho kikikamilika kitakuwa na uwezo wa kulaza wagonjwa 64 pamoja na nyumba za watumishi 24.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Injinia Emmanuel Kalobelo akisoma taarifa ya kituo hicho kwa Mhe. Makamu wa Rais. Kulia kwa Makamu wa Rais ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Injinia Stella Manyanya na kushoto kwake ni Mke wake Mama Asha Billal na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa Mhe. Hiporatus Matete.

Makamu wa Rais akikagua jengo la kituo hicho




AKIWA ZIARANI MKOANI RUKWA MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA MTAFITI BIGWA WA SOKWE DUNIANI AMBAYE PIA NI MTAALAMU WA MAZINGIRA IKULU NDOGO YA MPANDA

Si mwingine bali ni Jane Goodall ambaye ana zaidi ya miaka 73 mwanamama mtafifiti bigwa wa masokwe duniani kutoka Uingereza ambaye pia ni mtaalamu wa mazingira kwa pamoja Mhe. Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal anayeonyesha kitabu cha mwanamama huyo kiitwacho "Reason for Hope" kwa baadhi ya waandishi wa habari waliojumuika nao kwenye chakula cha jioni Ikulu ndogo ya Mpanda jana. Mama Jane ametumia zaidi ya miaka 40 ya utafiti wake katika Hifadhi ya Taifa ya Gombe iliyopo Mkoani Kigoma akitafiti maisha na tabia za Sokwe wanaopatikana kwa wingi katika mbuga hiyo.
.
Mtafiti Jane Goodall akimuonyesha Mhe. makamu wa Rais moja ya tabia za nyani ambayo ni salamu inayotumiwa na mnyama huyo ambaye hushika kichwa kama ishara ya maamkizi. Jane Goodal pia ni balozi wa mazingira na viumbe hai duniani katika kuhamasisha umuhimu wa uhai wa vitu hivyo pamoja na ustawi misitu.
Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Bllal akishika mdoli wa nyani ambao unamilikiwa na Mama Jane Goodgall kwa takribani miaka 15 sasa. Alisema kuwa anamiliki mdoli huo kutokana na hisia zake juu ya nyani ambao amekuwa akiwatafiti katika kipindi chote cha maisha yake.
Mama Asha Billal Mke wa Makam wa Rais na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa wakiwa wameshikilia mdoli huo ambao kwa hakika anavutia pamoja na historia yake.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Dkt. Rajab Rutengwe naye hakuwa nyuma kwani alimtia mkononi mdoli huyo wa kihistoria.
Mama Jane Goodall akikumbatiana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya kabla ya kuondoka katika Ikulu hiyo ndogo ya Mpanda jana usiku.
Picha ya pamoja kati Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal na Mama Jane Goodal. Kulia kwa Makamu wa Rais ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya, wa pili anayefuata na Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima. Kushoto kwa Mama Jane Goodall ni Mama Asha Billal Mke wa Makamu wa Rais na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Dkt. Rajab Rutengwe.

TAAARIFA YA MKOA WA RUKWA ILIYOSOMWA NA MKUU WA MKOA HUO KWA MAKAMU RAIS AMBAYE YUPO MKOANI HUMO KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU SABA

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akisoma taarifa yake ya Mkoa kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Mohammed Gharib Billal katika ukumbi wa Ikulu Ndogo ya Mpanda mara baada ya kuwasili kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku saba Mkoani Rukwa.

Mhe. Makamu wa Rais akifuatilia hotuba hiyo mstari baada ya mstari katika ikulu ndogo mjini mpanda

TAARIFA YA MKUU WA MKOA WA RUKWA KWA MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MHE. DKT. MOHAMMED GHARIB BILAL
KATIKA ZIARA YAKE MKOANI RUKWA
TAREHE 18 - 24 FEBRUARI, 2012.

Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
1.0. UTANGULIZI.

Mheshimiwa Makamu wa Rais, Awali ya yote napenda kuchukuwa fursa hii kukukaribisha wewe na ujumbe wako hapa Mkoani Rukwa. Sisi wananchi wa Mkoa wa Rukwa tunafarijika sana pindi tunapotembelewa na viongozi wa Kitaifa kwani tunajua wazi tutapata ushauri, maelekezo na maagizo kwa ajili ya kuboresha utendaji wetu wa kazi.

Mheshimiwa Makamu wa Rais, Taarifa hii inazungumzia habari za Mkoa wa Rukwa ambao ni pamoja na Mkoa mpya wa Katavi. Inaonyesha ulipo mkoa na umbile lake . Aidha, tunaelezea mafanikio na changamoto zilizomo katika sekta mbalimbali ikiwemo Elimu, Afya, maji, Kilimo, Ushirika, Uvuvi, Ardhi, Maendeleo ya jamii, Biashara, Viwanda, Miundombinu, Mawasiliano na Masuala mtambuka. Pia hatukusahau masuala ya Haki za Binadamu na Utawala bora.

MAKAMU WA RAIS AWASILI WILAYANI MPANDA LEO KWA ZIARA YA SIKU 7 MKOANI RUKWA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Billal akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Injinia Stella Manyanya mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mpanda leo kwa ziara ya kikazi ya siku saba Mkoani Rukwa.

Mhe. Makamu wa Rais akisalimiana na wananchi wa Mpanda mara baada ya kutua katika uwanja wa ndege wa Mpanda tarayi kwa kuanza ziara yake ya siku saba Mkoani Rukwa. Anayeongozana naye kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Injinia Stella Manyanya. Makamu wa Rais anategemea kufanya ziara yake katika wilaya zote tatu za Mkoa wa Rukwa ikiwepo Mpanda yenyewe, Nkasi na Mpanda ambapo atahitimisha ziara hiyo tarehe 24 Februari na kuelekea Mkoa jirani wa Mbeya

Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal akihutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika leo kwenye uwanja wa kashaulili wilayani Mpanda. Miongoni mwa mambo aliyosisitizia katika mkutano huo ni pamoja ujenzi wa mabweni katika shule za Sekondari kwa ajili ya wasichana kusaidia kuwaepusha na mimba za mashuleni. Aidha alisisitiza kuhusu upandaji miti kuepukana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.


MAKAMU WA RAIS KUFANYA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU 7 MKOANI RUKWA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mohammed Gharib Billal.

Makamuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mohammed Gharib Billal atafanya ziara ya siku saba Mkoani Rukwa ambapo itajumuisha pia Mkoa mpya wa Katavi. Ziara yake hiyo itaanza tarehe 18 na kumalizika tarehe 24 Februari 2012 akitokea mkoani Ruvuma.
Awapo Mkoani Rukwa atatembelea Wilaya zote tatu za Mpanda, Nkasi na Sumbawanga. Mpanda atakuwepo kuanzia tarehe 17 hadi tarehe 20 ambapo atapokea taarifa ya Serikali pamoja na Chama cha Mapinduzi. Aidha atafanya mkutano wa ndani katika Ofisi ya CCM Wilaya ya Mpanda na mikutano wa nje katika uwanja wa Kashaulili na Ofisi ya Tarafa Inyonga.
Pamoja na hayo atapata fursa ya kuweka jiwe la msingi katika kituo cha afya katika tarafa ya Inyonga na kufanya Mkutano wa hadhara. Akiwa njiani kuelekea tarafa ya Mpimbwe ataona Mbuga ya Wanyama ya Katavi ambapo ataweka jiwe la msingi katika Ghala la Stakabadhi Mazao na kukabidhi hati za kimila za umiliki wa ardhi 300 katika kijiji cha Mwamapuli.
Akiwa wilayani Nkasi kuanzia tarehe 20 Februari 2012 Makamu wa Rais atapokea taarifa ya ujenzi wa barabara za Mkoa wa Rukwa na taarifa ya Wilaya ya Nkasi. Atafungua miradi ya maendeleo ikiwepo nyumba ya watumishi wa Halmashauri, Jengo la Utawala Shule ya Sekondari Nkomolo, na Daharia Shule ya Sekondari Korongwe. Atafanya pia Mkutano wa hadhara katika kiwanja cha shule ya Sekondari Korongwe.
Akimaliza ufunguzi wa miradi hiyo, ziara yake itahamia katika Wilaya ya Sumbawanga ambapo atamalizia ziara yake na kuelekea Mbeya kwa ajili kuendelea na zoezi kama hilo ambalo linategemewa kufanyika katika nchi nzima.
Mhe. Makamu wa Rais atawasili Sumbawanga tarehe 22 Februari 2012 akitokea Nkasi ambapo atapokelewa na viongozi wa Chama na Serikali ngazi ya Mkoa na Wilaya. Baada ya kupokelewa atapewa taarifa fupi ya Chama na Serikali.
Awapo Sumbawanga atapata fursa ya kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ambapo ataweka jiwe la Msingi Jengo la ofisi ya Mkaguzi Mkazi Mkoa wa Rukwa na Jengo la benki ya CRDB. Atazindua Maghala ya kuhifadhi bidhaa bandarini yaliyopo Kasanga, Soko Jipya la Samaki Kasanga, na kampeni ya usafi katika Mji wa Sumbawanga “SUMBAWANGA NG’ARA” kwa kugawa vitendea kazi vya usafi.
Atapata pia fursa ya kusalimiana na wananchi katika maeneo yote ya miradi atakayotembelea ambapo atatembelea pia ngome ya “FORT BISMARK” iliyopo Kasanga na Kiwanda cha nyama cha SAAFI kinachomilikiwa na Mbunge Msataafu na mjasiriamali Ndugu Chrissant Mzindakaya.
Makamu wa Rais pia atafanya Mikutano wa hadhara katika viwanja vya Rukwa High School na Uwanja wa Mpira wa Laela. Atazungumza na wazee maarufu wa Wilaya ya Sumbawanga katika uwanja wa Ikulu Ndogo ya Sumbawanga.
Mhe. Makamu wa Rais atakamilisha ziara yake tarehe 24/02/2012 na kuondoka Sumbawanga kuelekea Mkoa jirani wa Mbeya ambapo atakuwa na ratiba ya ziara ya kikazi Mkoani humo.

KUTOKA RUVUMA LEO: MAKAMU WA RAIS ATOA TAMKO KUHUSU MRADI WA URANIUM - NAMTUMBO

Makamu Rais DKT Mohamed Ghalib Bilal akihutubia mamia ya wananchi wa kijiji cha Likuyu sekamaganga wilaya ya Namtumbo wakati alipofanya ziara katika mradi wa urani.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewahakikishia wakazi wa mkoani Ruvuma na Tanzania kuwa mradi wa mgodi tarajali wa Urani wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma utatekelezwa kwani una umuhimu kwa taifa.
Amesema hayo wakati akiongea na wafanyakazi wa mgodi huo unaomilikiwa na kampuni ya Mantra Tanzania kuwa serikali inafuatilia kwa makini kuona madini haya muhimu ya nalifaidisha Taifa
Aliongeza kuwa anao uhakika kuwa taratibu zote za hifadhi ya mazingira na usalama wa maisha ya wakazi wan aozunguka eneo hilo umetiliwa mkazo nwa Kampuni kwa kushirikiana na taasisi ya nishati ya atomiki Tanzania
.Aidha kwa upande wake Mkurugenzi wa Mantra Tanzania Asa Mwaipopo ameiomba serikali kuharakisha taratibu za kisheria ili mgfodi uweze kuanza hapo mwaka ujao kwa ujenzi na ifikiapo 2014 uzalishaji uanze ili ajira zipatazo 1600 wakati wa ujenzi wa mgodi na zingine 400 wakati wa uzalishaji ziweze kupatikana kwa watanzania na kusaidia kukuza uchumi.
Makamu wa Rais ya sampuli za urani kutoka kwa mjiolojia wa kampuni ya Mantra Emauel Nyamusika(kulia) wakati alipotembela mgodi tarajali.
Makamu wa Rais akipokewa na viongozi wa kampuni ya Mantra wakati alipowasili katika eneo litakalojengwa mgodi wa Uranium wilaya ya Namtumbo. (Picha na Revocatus A.Kassimba ofisi ya mkuu wa mkoa Ruvuma)

No comments:

Post a Comment