Dodoma. Spika wa Bunge, Anne Makinda
jana ni kama aliruhusu mvutano wa wazi baina ya wabunge wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) na wale wa Chadema ambao kila upande uliutuhumu upande
mwingine kwa kuhusika kwa viendo vya ugaidi.
Licha ya kutozungumzia suala hilo moja
kwa moja, lakini msingi wa tuhuma hizo ni kesi iliyofunguliwa
mahakamani dhidi ya Mkurugenzi wa Usalama wa Chadema, Willifred
Lwakatare ambaye anakabiliwa na makosa yanayomtuhumu kwa ugaidi.
No comments:
Post a Comment