Friday, March 29, 2013

Tamwa yataka waandishi wajue kujihami


Dar es Salaam. Wamiliki  wa Vyombo vya Habari nchini wametakiwa kutoa mafunzo ya kujihami na maadui kwa waandishi wa habari pamoja na mafunzo ya kuwajengea misingi na maadili ya uandishi bora wa kazi zao.

Hatua hiyo inatokana na  mfululizo wa matukio ya kutekwa, kuteswa na vitisho dhidi ya baadhi ya waandishi wa habara hapa nchini.

Akizungumza kwenye mkutano wa Wadau wa Habari, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi Habari Wanawake Tanzania (Tamwa), Valerie Msoka alisema, ipo haja sasa kwa wamiliki wa vyombo vya habari kutoa mafunzo kwa waandishi ili wawe na uwezo wa kujihami kwa hali ilivyo sasa.

Msoka alisema kwa jinsi hali ilivyo sasa ni vyema pia waandishi wakapewa mafunzo ambayo yanawapa mbinu jinsi gani wanaweza kupambana na misukosuko wakati wanapokuwa ndani na nje ya mahali pa kazi.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa, mbali na mafunzo hayo hali ya usalama  pia kwa waandishi bado ni kitendawili hapa nchini, hivyo wamiliki wanatakiwa kuwahakikishia usalama wao kikazi na kimahitaji.

Kwa upande wake, Profesa Nicholls Boas kutoka Chuo Kikuu cha Maryland Marekani, aligusia suala la mfumo wa vyama vingi kuwa ni changamoto kwa vyombo vya habari kutokana na kuweka mambo yaliyojificha wazi.

No comments:

Post a Comment