Wednesday, February 22, 2012

Pinda Naye Mtemi Usukumani

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mkewe Tunu wakicheza ngoma ya Watemi wa Kisukuma baada kupewa heshima ya kuwa Mtemi Masanja na Mkewe kuwa Ngole kwenye uwanja wa michezo wa Maswa wakiwa katika ziara ya mkoa wa Shinyanga Februari 20, 2012. Kushoto ni Mtemi Majebele ambaye ndiye alimpa heshima hiyo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)




 

RAIA mmoja wa Sweden aliyefahamika kwa jina la Gunnar ORG Gunnarson (19) amefariki dunia baada ya gari alilokuwa akisafiria kugongana na gari lingine. Kamanda wa polisi mkoani hapa, Thobias Andengenye alisema kuwa, tukio hilo limetokea febuari 18 mwaka huu majira ya saa 7;20 katika barabara ya Arusha-Moshi eneo la Kikatiti wilayani Arumeru mkoania Arusha. Alisema kuwa, siku tukio gari aina ya Range Rover lenye namba za usajili T 663 AYB lililokuwa likiendeshwa na Lusingu Lubero Mvungi (38) mkazi wa jijini Dar es Saalamu likitokea Arusha kuelekea Kia liligongana na gari aina ya Land Rover Defender lenye namba za usajili T 424 AYD mali ya Arunga Expedition Arusha Tours. Ambapo gari hilio lilikuwa likiendeshwa na Francis Paul (45) mkazi wa Sanawari lililokuwa likitoea Moshi kuja Arusha na kusababisha kifo cha Msweeden huyo ambaye alifariki akiwa anapakiwa kwenye ndege tayari kwa kwenda Nairobi kwa matibabu. Andengenye alisema kuwa, ajali hiyo ilitokea baada ya gari aina ya Range Rover kujaribu kulipita gari liliokuwa mbele yake na kisha kupoteza uelekeo na kwenda moja kwa moja kugongana na gari aina la Land Rover Defender. Aidha mbali na ajali hiyo kusababisha kifo hicho,pia ilisababisha majeruhi klwa kwa watu kumi na moja ambao ni John Halid (60) raia wa Denmark,Bjorn Hoj Glaetesthl (28)raia wa Denmark, ambao wote kwa pamoja wamepelekwa Nairobi kwa matibabu. Aidha alitaja majeruhi wengine kuwa ni Francis Paul(45) mkazi wa Sanawari ambaye amelazwa katika hospitali ya Mount Meru , Clemence Nicolous (32) mkazi wa Sakina ambaye alitibiwa na kuruhusiwa, Elibariki Nicolous (32) mkazi wa Sakina ambaye ametibiwa na kuruhusiwa. Aidha wengine ni Godfrey David (21) mkazi wa Lekulei ambaye ametibiwa na kuruhusiwa, Haruna Amir (31) mkazi wa Elikulei ambaye alitibiwa na kuruhusiwa, Sajun Mollel (20) mkazi wa Mianzini, naye alitibiwa na kuruhusiwa , Paulo Omben(34) mkazi wa Sakina ambaye alilazwa katika hospitali ya Mount Meru. Aliwataja majeruhi wengine kuwa ni Ombeni Masawe (26) mkazi wa Mianzini,ambaye amelazwa katika hospitali ya Mount Meru,na Lusingu Lubero Mvungi (38) mkazi wa Dar es salaam ambaye alitibiwa na kuruhusiwa. Aidha kutokana na tukio hilo,jeshi nla polisi mkoania hapa linaendelea kumshikilia dereva wa gari aina ya Range Rover ,Lusingu Lubero Mvungi (38) mkazi wa jijini Dar es salaam na kwamba pindi upelelezi utakapokamilika atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili. Wakati huo huo jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata watu wawili wajulikanao kwa jina la Linah Christopher( 50)na Elizabeth Christopher(40) wa maeneo ya ungalimited wakiwa na misokoto 314 ya madawa ya kulevya aina ya bangi Kamanda alieleza kuwa mafanikio hayo yalitokana na mafanikio ya taarifa zilizotolewa na raia mwema ambapo mara baada ya taarifa hiyo walikwenda moja kwa moja katika nyumba ya mtuhumiwa huyo na walipopekua walifanikiwa kupata bangi hiyo ikiwa imehifadhiwa katika mfuko wa plastiki Hata hivyo watuhumiwa hao walikiri kuwa walikuwa wamehifadhi bangi hiyo kwa ajili ya kuuza ambapo jeshi la polisi limeshawafikisha watuhumiwa hao mahakamani ili kujibu tuhuma ambazo zinawakabili..

No comments:

Post a Comment