Saturday, February 25, 2012

CPA Afrika Kufanyika Tanzania


Bunge la Tanzania kuwa mwenyeji wa Mkutano wa siku moja wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola kanda ya Afrika (CPA Africa). Mkutano huo utakaofanyika Mjini Arusha, kesho tarehe 24 Februari, 2012, ambapo kamati hiyo ya CPA Africa, inakutana nchini kujadili maswala mbalimbali ya chama hicho kwa kanda ya Afrika. Bunge la Tanzania ndio makao makuu ya chama hicho kwa kanda ya Afrika

Kamati hiyo itahudhuriwa na wajumbe wa kamati tendaji ambao ni:
Mhe. Rose Mukantabana (Mb) Rais wa Chama hicho kwa kanda ya Afrika na pia ambaye ni Spika wa Bunge la Rwanda
Mhe. Mninwa Mahalangu (Mb) Mwenyekiti wa kamati ya Utendaji wa Chama hicho ambaye pia ni Spika wa Bunge la Afrika Kusini
Mhe. Lindiwe Maseko (Mb) Makamu wa Rais wa CPA Afrika na pia ndiye Spika wa Jimbo la Gauteng, nchini Afrika Kusini

Mhe. Request Mutanga (Mb) Muweka Hazina wa CPA Afrika, na Mbunge kutoka Bunge Zambia

Mhe. Job Ndugai (Mb) Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, ambaye pia ndiye mwenyeji wa kamati hiyo hapa nchini,

Na Dr. Thomas Kashililah, Katibu wa Kanda wa chama hicho ambae pia ni katibu wa Bunge la Tanzania
Tanzania imekuwa makao makuu ya Kanda ya CPA Afrika tangu mwaka 2004, ambapo shughuli zote za chama hicho huratibiwa na sekretariat ya CPA ambayo ipo nchini Tanzania.
Imetolewa na Ofisi ya Bunge
Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Uhusiano wa Kimataifa
24, Februari, 2012
DAR ES SALAAM


Dk. Shein Awapongeza Halaiki

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein akipeana mikono na  kuwapongeza Walimu wa Mchezo wa Halaiki ambao walifanikisha Sherehe za Miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar huko Bwawani mjini Zanzibar.
Wanafunzi kutoka skuli mbalimbali ambao walifanikisha Sherehe za Miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiwa katika karamu maalumu ilioandaliwa kwa ajili ya kuwapongeza huko Bwawani Zanzibar

Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein wanne kutoka kushoto akiwa katika picha ya Pamoja na Walimu wa Halaiki ambao walifanikisha sherehe za Miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar kulia yake ni Makamo wapili wa Rais Balozi Seif Ali Idi.

No comments:

Post a Comment