Sasa imezinduliwa rasmi. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Meneja Mradi wa SWVR Bi. Aygen Aytac (kulia) na Afisa Mipango wa United Nation Volunteers (UNV) Bi. Stella Karegyesa kushoto.
Burudani kutoka kikundi cha International Youth Fellowship (IYF).
Na.Mwandishi wetu
Programu ya Wanajitolea ya Umoja wa Mataifa (UVN) leo imezindua ripoti ya kwanza juu ya hali ya kujitolea (SWVR) nchini Tanzania.
Ripoti hiyo inaangalia michango ya muhimu katika maeneo mbalimbali kama vilemaisha endelevu, kushirikishwa kwa jamii, mshikamano wa kijamii na kupunguza hatari ya majanga.
Ripoti hiyo vile vile inatoa mtazamo mbadala wa jamii bora na inaonyesha jinsi ya kusukuma mbele shughuli za kujitolea.
SWVR pia inaeleza umuhimu wa kupima viwango vya kujitolea ili kuvijumuisha kwenye mojawapo ya rasilimali kubwa za mataifa.
Kutokana na utafiti, kazi yakujitolea imechangia asilimia 1.5 ya pato la taifa (GDP) mwaka 2008, wakati wastani kwenye nchi zilizoendelea ni asilimia 0.7 ya GDP.
SWVR ilitolewa kwa jamii ya kimataifa kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 5 Disemba 2011 na kuzinduliwa kwenye nchini (80) duniani.
No comments:
Post a Comment